jeudi 9 octobre 2008

WAFUNGWA ZAIDI YA 15 WAJERUHIWA KATIKA JELA KUU LA MPIMBA MJINI BUJUMBURA
Katika uchunguzi ulioendeshwa kwenye jela kuu la Mpimba baada ya kutokea vurugu siku ya jumapili ambapo risase na hata bomu zilisikika jelani hapo, wafungwa wa tano wamegunduliwa kuhusika na vurugu hizo pia na kukutwa na shughuli za kutengeneza noti za magendo katika jela hilo la Mpimba. Duru kutoka kwenye jela kuu la Mpimba zimearifu kuwa kiini cha vurugu hizo ni mfungwa ambae aliagiza simu 4 za mkononi kwa mtu ambae aliekuwa amekwenda kumuona nduguye, baada ya kumpa pesa, na kuondoka ndipo akagunduwa kwamba noti zile alizo pewa sio noti halali, akamuwa kuzirudisha huko Mpimba. Alietowa pesa hizo akakana kurejesha simu, baadae ndipo wenzake walimuunga mkono na kuanzisha vurugu. Lakini hata hivo duru zaidi zimesema kuwa kiini cha vurugu hizo ni mzozo uliotokea bainaya wafungwa wakati wa kugawa simu za mkononi na pesa walizo zipata kutokana na suhghuli zao hizo za utengenezajiwa noti bandia. Polisi ililazimika kuingilia kati kwa kuvurumisha risase hewani kama zilivyo endelea kuarifu duru kutoka katika jela kuu hilo la Mpimba. Wafungwa zaidi ya 15 walijeruhiwa katika tukio hilo mmoja akiwa katika hali mbaya.

Aucun commentaire: