jeudi 9 octobre 2008

SERIKALI YA BURUNDI YAANDAA MABADILIKO KATIKA UTOWAJO MISHAHARA

Serikali ya Burundi imo mbioni kuandaa mradi mpya utaopelekea wafanyakazi wake kusalia nhini Burundi badala ya kufikiria kwenda ugenini aidha kutumikia mashirika ya wahisani ambayo hutowa donge nono zaidi kulikoni hapa nchini. Hii inatokana hasa na mshara mfinyu wanao pewa wafanyakazi wa serikali. Hayo yamefahamishwa na Pierre NTIRABAMPA Mkurugenzi mkuu kwenye wizara ya kazi wakati akiyajibu maswali ya waandishi habari katika kipindi mojawapo kilichokuwa kikitasmini hali halisi ya mfanyakazi wa serikali na jinsi gani ya kuboresha kazi na kupelekea mfanyakazi wa serikali apate nafuu katika utekelezwaji wa kazi zake. Kipindi hicho kilikuwa kimeandaliwa na muungano wa mashirika yanayo tetea haki za wafanyakazi COSYBU.

Aucun commentaire: