mercredi 20 mai 2009

KWA MARA YA TENA BARAZA LA SENETI LAONYESHA NIDHAMU NA UZALENDO


Baraza la Seneti limeidhisha majina yaliopendekezwa na rais wa jamuhuri Pierre Nkurunziza kwenye nyadhifa mbalimbali. Waziri wa ulinzi meja jenerali Germain Niyoyankana aliwasilisha kikaoni jina la Brigadia jenerali Ndegeya diomède ambae alipendekezwa na rais wa Burundi Pierre Nkurunziza kuwa kaimu mkuu wa majeshi ya Burundi. Brigadia jenerali Ndegeya Diomede aliidhinishwa kuwa kaimu mkuu wa majeshi ya Burundi. Upande mwigine, waziri wa mambo ya ndani Edourd Nduwimana aliwasilisha majina ya walipendekezwa na rais kuiwakilisha Burundi ugenini. Nibizi Isidore na Bashimiyubusa Denis kutoka chama FNL wamepasishwa kuiwakilisha Burundi ugenini. Elias Buregure wa chama CNDD-FDD ambae aliwahi kuwa mea wa jiji la Bujumbura kabla ya kuwa waziri mdogo wa kazi za serikali amekataliwa na wanaseneti kuiwakilisha Burundi ugenini kwa kushtumiwa katika kesi mbalimbali za ubadhilifu mali ya umma. kulingana na habari kutoka kwa wanaseneti Elias Buregure alijihusisha na rishwa katika utowaji viwanja vya ujenzi wakati alipokuwa waziri mdogo wa kazi za serikali ambae alipingana na waziri mkuu kwenye wizara hiyo katika kuchukuwa maamuzi. Baraza la seneti limeidhinisha pia majina ya ma gavana wa Mikoa ya Mwaro, Makamba na Cibitoke. Nahayo Fredine ataongoza Mkoa wa Mwaro ni kutoka chama FNL, Ntahitaja Térence ataongoza Mkoa wa Makamba ni kutoka chama CNDD–FDD, huku Bizimungu Simon akiidhishwa kuongoza Mkoa wa Cibitoke, akiwa ni mwanachama wa FNL.

KESI YA MAUAJI YA ALBINOS YASIKILIZWA NA MAHAKAMA KUU MKOANI RUYIGI.


Kesi ya watu 11 wanaoshukiwa kuendesha mauaji ya Albinos ilisikilizwa jumanne na mahakama kuu ya mjini Ruyigi. Kulingana na muandishi habari wa kituo cha Burundi cha kutawanyia ABP habari Mkoani Ruyigi Maurice Bukuru, kesi hiyo ilianza kusikilizwa tangu saa nne mchana ambapo halaiki ya watu walikuwa wamemiminika mahakamani kusilikiza kesi hiyo. Awamu ya kwanza ya kesi hiyo iliwahusisha watu 8 walioshutumiwa kuwamalizia maisha binti mmoja albinos aliejulikana kwa jina la Harerimana Violette alieuawa Septemba 8 mwaka jana, pamoja na mtoto mwgine alieuawa katika kijiji cha Kinyinya na bwana mmoja albinos alieuawa Bweru. Washukiwa wengine wanashutumiwa kuhuika na jaribio la mauaji ya Albinos. Washukiwa hao walitajwa na wafungwa ambao walikatiwa kifungo cha maisha jela ambao wanazuiliwa katika jela kuu la Ruyigi. Wafungwa hao wanaozuiliwa jela walihusika na mauaji ya binti mmoja Albinos na kuuza viungo vya mwili mtu ajulikanae kwa jina Richard Adelin wa tarafa ya Cendajuru Mkoani Cankuzo ambae yuu huru hadi sasa. Katika kesi hiyo Nyabenda Elie maharufu Bihoro alikiri kuhusika katika mauaji hayo huku wengine wakikana kuhusika moja kwa moja. Hakimu mkuu wa jamuhuri Mkoani Ruyigi Nicodème Gahimbare aliwakamata kinaga ubaga mwezi march iliopita watu 11 wakiwa na viongo vya Albinos. Mkoa wa Ruyigi ndio ambao ulioorodhesha idadi kubwa ya mauaji ya Albinos waliouawa tangu kuanzishwa kwa visa vya mauaji ya Albinos vilivyo anzia nchini Tanzania na kutanda hadi nchini Burundi. Tangu kukamatwa kwa mtandao huo wa wahalivu wa mauaji ya Albinos Mkoani Ruyigi mwezi march hakuna kitendo kiovu kama hicho ambacho kimekwisha ripotiwa hadi leo.