SHEREHE ZA ID-IL FITRI ZAFANYIKA VEMA LICHA YA SERIKALI KUTOKUWEPO
Kama ilivyokuwa kawaida kila mwaka, jamii ya waislam nchini Burundi COMIBU huitolea serikali taarifa katika maadhimisho ya siku kuu ya Idil Fitri inayo maanisha mwisho wa mwezi mtukufu wa Ramadhani. hata hivo kumekuwa na mtafaraku kila mwaka inapo wadia kufungua mwezi ambapo inafikia waislam kufunga siku 30 ao 29, hili linaeleweka, lakinikwa sasa kumekuwemo na mambo ya siasa ndani yake. waislam walifurika kwa wingi kuendesha ibada yao ya sala ya laidi kama ilivyokuwa kawaida. jumuia ya waislam nchini Burundi COMIBU iliwatangazia waislam viwanja maalum ambavyo vitaendeshewa ibada na ma shekh ambao wataendesha ibada hiyo. inakubalika wazi kwamba sherehe rasmi hufanyika kila mwaka Mtaani Jabe, eneo kubwa linalo kusanyikia waumini wengi. mwaka huu kama ilivyo staajabisha wengi sherehe rasmi ziligeuzwa na kupelekewa kwingine. serikali ilimtuma muwakilishi wake huko kwingine. hili halikupelekea sherehe kutofana, badala yake sherehe kwenye uwanja wa idi zilipendeza kiasi kwamba Cheikh Issa Salum BAGORIBARIRA alikuwa ameandaa hutba yake fupi yenye kujawa na ujumbe mzito, ilimalizika huku waumini wakihitaji aendelee. Waumini wa kiislam wamepinga kuendesha malumbano kutokana na hilo kwa kuwa kama walivyo ieleza blogi hii, wanayo matatizoi mengine ndani ya jamii ambayo yawakabili, na kuzidi kuwa hilo ni lidogo, kwa kuwa Uislam ulikuwepo tangu kabla ya utawala uliopo, na Uislam utasalia ulipo huku utawala uliopo ukitoweka.
Aucun commentaire:
Enregistrer un commentaire