jeudi 25 septembre 2008

WARUNDI 20 WALIOFUKUZWA NCHINI TANZANIA WAWASILI MKOANI RUTANA KUSINI MWA BURUNDI


Raia takriban 20 waliofukuzwa nchini Tanzania, wamewasili jana jumatano asubuhi tarehe 24/9/2008 katika mkoa wa Rutana kusini mwa Burundi bada ya kutembea kwa mguu kwa muda wa siku 15. Raia hao wengi wao ni watoto na wanawake waliokuwa wakiishi nchini Tanzania tangu mwaka 1995 katika kijiji cha Bukiriro wilaya ya Ngara Mkoani Kagera. Raia hao walifukuzwa nchini Tanzania tangu tarehe 9 mwezi wa 9 na wamedai kuwa wazaliwa wa mikoa ya Cibitoke na Ngozi na kwamba walifurushwa na watu wa jamii ya wanangambo waliowapora mali na vitu vyao.
Shughuli za ujenzi wa soko la Buyenzi zimekamilika. kinacho salia ni shirika la mamlaka ya maji na umeme REGIDESO paomja na manispaa ya jiji la Bujumbura kushughulikia maswala ya umeme na maji katika soko hilo muhimu kwa uchumi wa nchi. hayo yamethibitishwa na Anatole MPERAMIHIGO ambae alikuwa akisimamia shughuli za ujenzi wa soko hilo. Lakini hata hivo kumekuwa na uvumi kwamba shughuli za ujenzi wa soko hilo la Ruvumera zilikamilika tangu kitambo, uzinduzi rasmi unacheleweshwa kutokana na hali ya viongozi wa kuu serikali kujipa viwanja zaidi ya vitano kila mmoja ambapo waliokutwa katika soko hilo kabla hata halijakarabatiwa huenda wakakosa viwanja.
MSEMAJI WA PALIPEHUTU/FNL ATHIBITISHA KWAMBA WANAO MA AFISAWA WA KIJESHI KATIKA KUNDI LAO.

Akizungumza na redio Burundi jumatano hii tarehe 24/9/2008, msemaji wa palipehutu/FNL Pasteur HABIMANA amesema kuwa katika idadi walioitowa ya jeshi lao wanao ma afisa wakuu wa jeshi, ambao hawahitaji mafunzo ya kuwa ma afisa. hayo ni baada ya serikali ya Burundi kutowa taarifa ambamo iliwataka vijana kujiunga na chuo kikuu cha kijeshi ISCAM wakiwemo vijana kutoka kundi hilo la palipehutu/FNL. msemaji huyo wa FNL alisema kuwa majadiliano baina ya seriklai ya Burundi na kundi hilo yaendelea vema licha ya kasoro kadhaa ambazo zimekuwa zikijitokeza. miongonimwa kasoro hizo amesema Pasteur HABIMANA ni kuitwa kwa kundi lao palipehutu/FNL. amezidikuwa haoni pengamizi popote lilipokwa kuwa kila wanapo itishwa katika mikutano aidha kongamano lolote huitwa kama palipehutu FNL, alisema na hata wakati wa mechi baina ya wanajeshi wa Burundi na wapiganaji wa kundi lao waliitwa kuwa wapiganaji wa palipehutu FNL.

mercredi 3 septembre 2008

POLISI YA USALAMA WA RAIA YAMMALIZIA MAISHA JAMBAZI BAADA YA KUWAPORA HABIRIA KWENYE BARABARA ITOKAYO BUJUMBURA KUELEKEA GATUMBA
Majambazi wenye silaha waliendesha mtego siku ya jumamosi tarehe 30/8/2008, kwenye barabara itokayo mjini Bujumbura kuelekea tarafani Gatumba. basi moja la habaria lilianguka kwenye mtego huo. habiria waliokuwemo ndani ya basi hilo waliporwa pesa, simu za mkononi na vitu mbalimbali vya thamani waliokuwa navyo. baada ya shambulio hilo, jeshi la taifa eneo hilo liliingia kati na kumuua jambazi mmoja ambae alikuwa amevalia sare za jeshi la Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo. Hata hivo raia wa Gatumba waliokuja kushuhudia tukio hilo walithibitisha kwamba jambazi huyo alieuliwa ni mkaazi wa kata ya Gatumba. mnamo siku zote hizi za nyuma kumekuwa na hujuma mbalimbali ambazi zimekuwa zikiendeshwa na majambazi wenye silaha katika barabara tofauti zinazo toka mjini Bujumbura kuelekea mikoani.