Waziri wa mambo ya ndani amewapigia maarufu magavana kutoa ruhusa jumamosi wakati wa shughuli za usafi. Waziri Edouard Nduwimana ameiambia idhaa hii kwamba hatua yake imetokana na wananchi wengi kuomba ruhusa za udhuru wa kusafiri jumamossi na hivo shughuli za usafi kuonekana zikipuuziwa. Amewashauri wananchi hasa wasafiri badala ya kun’gan’gania kuomba ruhusa za jumamossi waandae mikakati ya safari zao mapema kuhakikisha kwamba wamefika katika maeneo wanakokwenda kabla au baada ya shughuli za usafi za jumamossi asubuhi. Aidha waziri huyo wa mambo ya ndani amesema kwamba iwapo udhuru wa kuomba idhni utaonekana una umuhimu mkubwa kama shughuli za musba au safari za ndege, basi wakuu wa mikoa watajadili hilo na kumpa ruhusa muhitaji.
jeudi 27 août 2009
VIONGOZI NCHINI BURUNDI WAMESHSREHEKEA MIAKA 4 KITITI WAKIWA KWENYE UTAWALA
Jana Agosti 26 viongozi walioteuliwa kwa misingi ya kidemokrasia nchini Burundi walitimiza miaka 4 kititi wakiwa kwenye utawala, baada ya uchaguzi wa mwaka 2005. Rais wa jamuhuri Pierre Nkurunziza nae pia ametimiza miaka 4 akiwa kwenye usukani wa kuiongoza Burundi. Rais Nkurunziza alizungumzia katika hutba yake jana kuhusu mustakabali mzima wa kuiongoza nchi na matatizo anayo kumbana nayo pia na mipango ijayo. Miongoni mwa yaliotekelezwa na serikali yake ni pamoja na mpango wa kudumisha amani nchini Burundi ambapo wakati huu nchini Burundi hakuna tena makundi ya uasi. Katika mipango ijayo Rais Nkurunziza amefahamsiha kuwa uchaguzi utafanyika kama ilivyo pangwa na katiba ya Burundi ameahidi kuwa uchaguzi utafanyika katika hali tulivu na ya muafaka, ameomba wale wanaopendelea kufuatilia shughuli za uchaguzi wa Burundi wangeanza mapema wakati huu. Kuhusu secta ya Afya na jamii rais Nkurunziza alitangaza mpango wa kutowa tiba kwa akinamama kuanzia mwanzo wa ujauzito hadi wanajifungua na baadae. Rais Nkurunziza ametumia fursa hiyo kukemea baadhi ya ma dactari na wauguzi ambao wamekuwa wakitowa kauli mbaya kutokana na mpango huo wa kutowa tiba pasina malipo.
mardi 18 août 2009
BEI YA MAFUTA YA GARI YAPANDA KWA MARA YA TENA
Serikali ya Burundi imechukuwa hatuwa ya kupandisha bei ya mafuta ya gari. Mafuta aina ya essence imepanda kutoka franka 1650 hadi 1700 lita moja huku mafuta aina ya Mazout ikipanda kutoka franka 1600 hadi 1650. hatuwa hii imechukuliwa wiki mbili baada ya kuchukuwa uamuzi kama huo, hali ambayo iliopelekea bei ya nauli za usafuri kwa abiria wanaosafiri kutoka katika tarafa mbalimbali na hata mikoani kupanda. Shirika linalo tetea haki za wanunuzi ABUCO limeihimiza serikali kufuatiliya kwa karibu bei ya mafuta ya petroli na kukomesha kuongeza bei ya mafuta hayo kwani husababisha ongezeko pia la bei ya bidha nyingine mahitajio.
ALEXIS SINDUHIJE MWENYEKITI WA CHAMA MSD ATAKIWA KUTOWA USHAHIDI DHIDI YA MATAMSHI YAKE

Mkuu wa chama MSD Alexis Sinduhije Jumanne Agosti 18 ameripoti mbelele ya hakimu mkuu wa jamuhuri katika jiji la Bujumbura akitakiwa kutowa ushahidi juu ya matamshi yake kuhusiana na kuwepo na njama ya kuunda kundi la vijana wa kabila la kitutsi lenye lengo la kuwamaliziya maisha baadhi ya watu nchini wakiwemo viongozi, ili baadae wavikwe dhamana wafuasi wa chama MSD. Na kwamba mpango huo umekuwa ukiandaliwa na idara ya upelelezi.
POLISI MKOANI MURAMVYA YAFAULU KUKAMATA NOTI ZA MAGENDO ELFU 30 ZA ELF 5
Noti za magendo 30 za elfu 5 zilikamatwa Bugarama katika mkoa wa Muramvya. Noti hizo zilikamatwa zikiwa na bwana jean Minani aliekamatwa na askari polisi, na kudai kuwa pesa hizo alizipata baada ya kuuza ngombe. Lakini majirani wa mtu huyo wamekanusha kuwa hajawahi kuuza ngombe wala kufuga, na kwamba mtu huyo amekuwa akitowa noti hizo za elfu 5 bandiya ili kununuwa pombe. bwana huyo amewekwa kizuizinii mkoani hapo Murambya.
Viongozi tawala Mkoani hapo Muramvya wamewatolea mwito wananchi kuwa makini sana wanapo pokea noti.
Viongozi tawala Mkoani hapo Muramvya wamewatolea mwito wananchi kuwa makini sana wanapo pokea noti.
vendredi 14 août 2009
MIAKA 5 IMEMALIZIKA TANGU YATOKEE MAUAJI YA WATU ZAIDI YA 160.
Wakimbizi Banyamulenge kutoka RDC alhamis hii Agost 13 wameadhimisha mwaka 5 tangu kuuawa kikatili wakimbizi 161 katika kambi ya Gatumba waliko kuwa wamepewa hifadhi , ilikuwa Agosti 13 mwaka wa 2004. Walionusurika katika mauwaji hayo wameitaka serikali ya Bdi na jamii ya kimataifa kufahamisha matokeo ya uchuguzi uliofanyika ili sheria iweze kufuata mkondo wake., amebaini hayo David BaNoGe msemaji ya walionusurika katika mauwaji hayo ya Gatumba. sherehe za kuweka mashada ya mauwa kwenye kaburi la pamoja waliko zikwa wahanga wa mauwaji hayo, zimeanfayika ambapo baadae hutba mbalimbali zilitolewa.
Itakumbukwa kuwa wapiganaji zamani wa FNL walithibitisha kuhusika na mauaji hayo na kusema kwamba walikuwa wakipambana na majeshi ya Burundi, na baadae wakaaza kushambuliwa na makombora kutoka katika kambi hiyo, hivo kujibu, na baadae kukuta kulikuwepo makundi ya wanajeshi waliokuwa na nia ya kuendesha mashambulizi mjini Uvira. Msemaji wa FNL zama hizo Pasteur Habimana alithibitisha hilo na kubaini kuwa kulikuwepo na vifaa vinavyo tumiwa kwa kuunguza majumba aina ya unga, ambavyo vilivyo sababisha watu hao wasiokuwa na hatia kuteketea. Serikali ya Burundio zama hizo ilikanusha madai hayo na kushutumu moja kwa moja makundi ya wa wapiganaji wa Rwanda wa FDLR na Mai Mai kuhusika na mauaji hayo. Miaka 5 sasa imemalizika hakuna ukweli wowote kuhusu mauaji hayo. Jamii ya kimataifa na serikali za Burundi na DRC kwa nini zimesalia kimya ? Nani aulizwe ao nani alaumiwe ?
Itakumbukwa kuwa wapiganaji zamani wa FNL walithibitisha kuhusika na mauaji hayo na kusema kwamba walikuwa wakipambana na majeshi ya Burundi, na baadae wakaaza kushambuliwa na makombora kutoka katika kambi hiyo, hivo kujibu, na baadae kukuta kulikuwepo makundi ya wanajeshi waliokuwa na nia ya kuendesha mashambulizi mjini Uvira. Msemaji wa FNL zama hizo Pasteur Habimana alithibitisha hilo na kubaini kuwa kulikuwepo na vifaa vinavyo tumiwa kwa kuunguza majumba aina ya unga, ambavyo vilivyo sababisha watu hao wasiokuwa na hatia kuteketea. Serikali ya Burundio zama hizo ilikanusha madai hayo na kushutumu moja kwa moja makundi ya wa wapiganaji wa Rwanda wa FDLR na Mai Mai kuhusika na mauaji hayo. Miaka 5 sasa imemalizika hakuna ukweli wowote kuhusu mauaji hayo. Jamii ya kimataifa na serikali za Burundi na DRC kwa nini zimesalia kimya ? Nani aulizwe ao nani alaumiwe ?
BUNGE LA BURUNDI LAIDHINISHA MUSWADA WA SHERIA UNAOPIGA VITA MATUMIZI YA SILAHA ZA MAANGAMIZI
Bunge la Burundi limeidhinisha alhamis hii Agost 13 muswada wa sheria ya kimataifa inayo piga marufuku matumizi ya silaha za maangamizi makubwa na makombora mengine madogo madogo yanayo weza kuripuka pindi mtu anapo yasogeleya. Silaha hizo zinao uzito wa kilo 20, na zaweza pia kuripuka kabla ya kuwasili pale yalipo elekezwa. Waziri wa ulinzi wa Burundi Germain Niyoyankana alikuwa mgeni wa heshma bungeni kufafanuwa mswada huo wa sheria. Wabunge wamemuuliza umuhimu wa usainiwaji sheria hiyo kwa Bdi, waziri wa ulinzi amejibu ya kuwa sheria hiyo ni muhimu ktk lengo la kujikinga na kujihami pindi Bdi ipo kuwa imeshambuliwa. Jumla ya wabunge 98 waliohudhuria kikao hicho cha bunge, wabunge 98 wameipasisha huku mmoja akisaliya pasina kubaini msimamo wake.
Inscription à :
Articles (Atom)