jeudi 9 octobre 2008

HATUWA KADHAA ZACHUKULIWA ILI KUWALINDIA USALAMA MA ALBINOS
Viongozi waliokuwa wkikutana mjini Ruyigi juzi jumanne na jumatano katika mkutano na wa wakilishi wa ma zeruzeru,hatimae wameazimia hatuwa za muda ili kuwalindia uslama mazeuzeru ambao wanakabiliwa na uslama mdogo Mkoani Ruyigi na hata Mikoa mingine mathalan Cankuzo. Kwa mujibu wa kiongozi wa shirika la ma albinos nchini nchini Burundi Kazungu Kassim, amesema kwamba miongoni mwa hatuwa zilizo chukuliwa ni kuwapatishia nyumba mojawapo katika tarafa ya Ruyigi ambako watalindiwa usalama zaidi. Kiongozi huyo aliwatolea mwito ma albinos popote pale walipo kutosita kujisalimisha kwenye makao makuu ya tarafa pindi tu watapojihisi kuwa usalama wao upo hatarini. Kiongozi huyo aliendelea kusema, wakati huu wanahitaji misaada ya kukidhi mahitaji ya ma albinos hao ambao wamekusanywa pamoja. Kiasi ma albinos 48 ndio ambao wanahesabiwa kueshi katika Mkoa huo wa Ruyigi. Kwa sasa wamekwisha kusanyika ma albinos zaidi ya 10 kwenye nyumba hiyo iliochukuliwa kama kituo cha kuwahifadhi ma albinos.

Aucun commentaire: