VYAMA VYA KISIASA NCHINI BURUNDI VYA IFASIRI HATUWA YA KUZUIA MIKUTANO YA HADHARA KUWA IMEPITWA NA WAKATI
Waziri wa mambo ya ndani na maendeleo ya vijiji Venant Kamana alitangaza kwamba hakuna mikutano yoyote ile aidha maadamano yoyote ya vyama vya kisiasa ya hadhara yatakubaliwa tena kuendeshwa holela bila kuwa na kibali rasmi, na kwamba siku za maadamano ni jumamosi na jumapili. Maandamano aidha mikutano uya siku ya jumamosi yatakubaliwa kuazishwa saa tano hadi saa kumi na mbili jioni, na siku ya jumapili ni kuanzia saa mbili asubuhi hadi saa kumi na mbili jioni. Kama alivyo kazia tangazo lake hilo waziri wa mambo ya ndani amesema kuwa hii ni kuepusha vurugu ambazo zaweza kujitokeza katika siku zijazo kutokana na mikutano ya vyama vya kisiasa. Mkurugenzi mkuu kwenye wizaraTérence Mbonabuca, upande wake alisema kuwa hatuwa hiyo ilichukuliwa baada ya kujadiliana na viongozi mbalimbali wa vyama vya kisiasa. hatuwa hii imepokelewa kwa shingo upande na vyama vya kisiasa. Mwenyekiti wa chama SAHWANYA FRODEBU Léonce NGENDAKUMANA amesema kwamba hatuwa hiyo anayo jaribu kuchukuwa waziri wa mambo ya ndani na maendeleo ya vijiji ni ya zamani wakati ambapo Burundi ilikuwa ndio bado inaingiza mguu katika mfumo wa kidemokrasia ambapo serikali ya zama hizo iliamuru kupinga maandamano na mikutano ya vyama vya kisiasa lakini wakati huu Burundi imepiga hatuwa kubwa, hakuna budi kuendelea mbele kuliko kurejea nyuma, na kwamba hakuna sheria ya kiwaziri ambayo yaweza kufuta sheria ya katiba aidha sheria kuhusu vyama vya kisiasa. Léonce NGENDAKUMANA ameendelea kusema kua iwapo waziri wa mambo ya ndani ameona umuhimu wa kubadili badhi ya sheria ni kusukuma mapendekezo yake bungeni ili yajadiliwe. Kiongozi huyo amesema chama FRODEBU kitapinga hatuwa zozote zile za kuzuia mikutana na maadamano ya vyama visivyo unga mkono chama kilicho madarakani. maoni kama hayo yalitolewa pia na msemaji wa chama CNDD Francois BIZIMANA
Aucun commentaire:
Enregistrer un commentaire