Hali ya kutoelewana imekuwa ikijitokeza mnamosiku zote hizi za nyuma baina ya viongozi wa kanisa la kimethodist unies katika sehemu mbalimbalia za Burundi.Tukio la karibuni ni la Hivi majuzi Mkoani Gitega viongozi wa kanisa hilo walitwangana ngumi na kuzusha vurumai na hivo kuvuruga usalama wa raia katika Mkoa huowa Gitega, pindi walifikia hali ya kuvurumishiana mawe. Kulingana na waziri wa mambo ya ndani Edouard Nduwimana amesema kuwa inaskitishwa kuona watu ambao wangelipooza nyoyo za waumini kwa kuwahutubia neno la Mungu na kuleta maendeleo, sasa ndio ambao wanavuruga usalama. Waziri huyo wa mambo ya ndani amesema kuwa walichukuwa hatuwa ya kufunga kanisa hilo baada yakutokea vurumai hizo hadi pale juhudi za upatanishi zitafikia tamati, waliopigana nao waliwekwa nguvuni na vyombo vya uslama kabla ya kufunguliwa faili na vyombo vya sheria. Waziri Edourd Nduwayo ameomba viongozi wa makanisa kuheshimu sheria zao na watakumbwa na sheria ya mwaka 1992 inamaanisha kwamba watachukuliwa hatuwa kama mashirika mengine. Amesisitizia viongozi hao wa makanisa kuheshimu sheria na kuweka mbele maendeleo na marisdhiano ya wananchi badala ya kutia mbele vyeo. Waziri huyo wa mambo ya ndani amesema kuwa kwa sasa watu wamekuwa wakishangazwa na kujiuliza vipi wahubiri sasa ndio wafia vyeo wakati cheo ni dhamana. Amesema wamo mbioni kuendesha mikutano na viongozi mbalimbali wa makanisa ili wawahamasishe kuhusu kutia mbele maridhiano badala ya kufarakiana na ilihali ni viongozi.
mercredi 18 février 2009
VIONGOZI WA KANISA WAFIA MADARAKA MBELE YA WAUMINI WAO
Hali ya kutoelewana imekuwa ikijitokeza mnamosiku zote hizi za nyuma baina ya viongozi wa kanisa la kimethodist unies katika sehemu mbalimbalia za Burundi.Tukio la karibuni ni la Hivi majuzi Mkoani Gitega viongozi wa kanisa hilo walitwangana ngumi na kuzusha vurumai na hivo kuvuruga usalama wa raia katika Mkoa huowa Gitega, pindi walifikia hali ya kuvurumishiana mawe. Kulingana na waziri wa mambo ya ndani Edouard Nduwimana amesema kuwa inaskitishwa kuona watu ambao wangelipooza nyoyo za waumini kwa kuwahutubia neno la Mungu na kuleta maendeleo, sasa ndio ambao wanavuruga usalama. Waziri huyo wa mambo ya ndani amesema kuwa walichukuwa hatuwa ya kufunga kanisa hilo baada yakutokea vurumai hizo hadi pale juhudi za upatanishi zitafikia tamati, waliopigana nao waliwekwa nguvuni na vyombo vya uslama kabla ya kufunguliwa faili na vyombo vya sheria. Waziri Edourd Nduwayo ameomba viongozi wa makanisa kuheshimu sheria zao na watakumbwa na sheria ya mwaka 1992 inamaanisha kwamba watachukuliwa hatuwa kama mashirika mengine. Amesisitizia viongozi hao wa makanisa kuheshimu sheria na kuweka mbele maendeleo na marisdhiano ya wananchi badala ya kutia mbele vyeo. Waziri huyo wa mambo ya ndani amesema kuwa kwa sasa watu wamekuwa wakishangazwa na kujiuliza vipi wahubiri sasa ndio wafia vyeo wakati cheo ni dhamana. Amesema wamo mbioni kuendesha mikutano na viongozi mbalimbali wa makanisa ili wawahamasishe kuhusu kutia mbele maridhiano badala ya kufarakiana na ilihali ni viongozi.
vendredi 13 février 2009
WIZI WA KUTUMIA SILAHA WAKITIHIRI KUSINI MWA BURUNDI
Usalama mdogo unaripotiwa katika kiji cha Canda tarafani kayogoro katika mkoa wa kusini wa Makamba .Duru tawala zinasema wizi wa kutumia silaha na mitego ya kuvizia magari vimeibuka katika sehemu hiyo. Gavana wa mkoa wa makamba Pasteur BUCUMI ameiambia idhaa hii kuwa hivi majuzi polisi imefaulu kukamata guruneti , silaha moja na sare za kijeshi kwenye msako uliofanyika tarafani hapo Kayogoro. Ameongeza kuwa uchunguzi uliofanywa unaonyesha kuwa wahalifu wanatokea katika mkoa jirani wa Bujumbura vijijini.
jirani ya hapo tarafani Rumonge mkoani Bururi, Raia mmoja mfanyabiashara kwa jina Amissi Mpitabakana ameporwa kitita cha pesa zinazokadiriwa miloni 5 na laki 3 za shillingi , sarafu ya Tanzania. Kulingana na muandishi wa habari wa shirika la Burundi la habari ABP sehemu hiyo, mfanyabiashara huyo alikuwa anajiandaa kusafiri na kitita hicho hadi Tanzania kwenda kulangua bidhaa za kuuza.
jirani ya hapo tarafani Rumonge mkoani Bururi, Raia mmoja mfanyabiashara kwa jina Amissi Mpitabakana ameporwa kitita cha pesa zinazokadiriwa miloni 5 na laki 3 za shillingi , sarafu ya Tanzania. Kulingana na muandishi wa habari wa shirika la Burundi la habari ABP sehemu hiyo, mfanyabiashara huyo alikuwa anajiandaa kusafiri na kitita hicho hadi Tanzania kwenda kulangua bidhaa za kuuza.
MASHIRIKA YA KICHINA YAZIDI KUJIZATITI NCHINI BURUNDI
Machimbo ya Nishati ya Nickel ya Musongati kusini mwa nchi yamekabidhiwa shirika lipya la SAMANCOR kutoka Uchina. Serikali ya Burundi ndio tu imetoa kwa shirika hilo kibali cha utafiti na shughuli za machimbo zimepangwa kuanza mnamo kipindi cha miaka miwili ijayo.
Hayo yamefahamishwa na waziri wa BDI wa nishati na madini Samuel Ndayiragije. Waziri huyo amesema uwanja huo wa machimbo ya madini ya Nickel ulikuwa wazi baada ya serikali ya Burundi kuvunja kandarasi ya shirika la Andover tangu mwaka 2007.
Hayo yamefahamishwa na waziri wa BDI wa nishati na madini Samuel Ndayiragije. Waziri huyo amesema uwanja huo wa machimbo ya madini ya Nickel ulikuwa wazi baada ya serikali ya Burundi kuvunja kandarasi ya shirika la Andover tangu mwaka 2007.
WAALIMU WA BUTERERE WAANZISHA MGOMO
Waalimu wa shule za msingi na upili tarafani Buterere kaskazini mwa jiji la Bujumbura wameanzisha mgomo wa kususia kutoa visomo wakidai wapewe kwanza viwanja vya ujenzi walivyoahidiwa na serikali. Waalimu hao wanaojumuika kwenye mashirika ya waalimu ya STEB na CONAPES wanaonyeshea hasa kidole Baraza la madiwani tarafa hapo ,kugawa viwanja hivyo kwa watu binafsi badala ya kuwapatishia waalimu. Mwenzangu Karim Nkeshimana amezungumza na Jean Bosco Ndarusanze , mwalimu wa shule la upili wa Buterere. Pamoja na mgomo huo , kazi ya dharura imekuwa inafanywa ikiwa ni pamoja na kutoa visomo kwa wanafunzi wa madarasa ya sita na ya kumi yanayotahiniwa kitaifa. Tumejaaribu kuwasiliana na wakuu wa tarafa ya Buterere kutoa muanga zaidi kuhusiana na hali hiyo pasina mafaanikio.
WAGANGA NA WAUGUZI WATISHIA KUREJEA MGOMONI
Vyama vya wauguzi na waganga vimetishia kuanzisha tena mgomo kuanzia jumatatu ijayo,.Mkuu wa chama cha madakatari Pierre Claver Hajayandi amesema kwamba mapatano yaliofikiwa kati yao na serikali hayakutekelezwa .Nae mmoja wa wapatanishi kwenye ugomvi kati ya serikali na mashirika hayo ya waganga, Rais wa zamani wa Burundi Sylvestre Ntibantunganya ameahidi kutoa muanga zaidi kuhusiana na mzozo huo jumamosi Februari 14.
USALAMA BADO WAYUMBISHWA RUYIGI
Gari ya hospital ya mkoa wa cankuzo imeanguka jana jioni alhamisi 12.2.209 kwenye mtego wa watu wenye silaha tarafani bweru katika mkoa wa mashariki wa Ruyigi. Kulingana na muandishi wa shirika la Burundi la habari sehemu hiyo watu waliokuwa wanavalia sare za kijeshi wamepora fedha inayokadiriwa laki sita na mtambo wa kemikali unaokadiriwa kuwa na thamani ya franka milioni 5.
Inscription à :
Articles (Atom)