dimanche 5 octobre 2008

USALAMA

WALINZI 3 WA SHIRIKA LA KK SECURITY WATIWA MBARONI KWA KUSHUKIWA KUHUSI NA WIZI WA PIKIPIKI 4 MKOANI RUTANA.

Polisi ya usalama wa raia Mkoani Rutana ilifaulu kukamata pikipiki 4 mpya katika usiku wa kuamkia ijumaa, zilizo ibiwa katika usiku huo kwenye shirika la GTZ Mkoani Rutana. Watu 3 wa shirika la Ulinzi la KK Security na mhusika wa shuhuli za kunyunyuzia maji bustani katika shirika la GTZ wamewekwa mbaroni kwa kushukiwa kuhusika na wizi wa pikipiki hizo mpya ambazo zilikamatwa kwa mchango mkubwa wa raia Mkoani hapo. Kama alivyo fahamisha afisaa wa polisi ya usalama Mkoani Rutana Sylvestre NZOHABONAYO, waliipokea simu kutoka kwa raia ambae aliwafahamisha kuona hali ya sintofahamu ambapo pikipiki mpya zinasukumwa usiku wa saa nne unusu, zikitokea kwenye makao makuuya shirika la GTZ Mkoani Rutana zikielekezwa katika kata ya Birongozi. Kiongozi huyo aliamuru kikoso chake kuripoti haraka, wezi hao walifaulu kitimka baada ya kuwaona askari polisi. Baadae polisi walipojielekeza kwenye shirika hilo la GTZ, ndipo walinzi wakajaribu kutimka bila mafaanikio, kwa kuwa, polisi ilikuwa imetanda eneo zima la shirika hilo. Baada ya kuendesha msako zaidi ndipo iligunduliwa pikipiki nyingine ambayo ilikuwa kweye kituo cha mafuta mkoani hapo, huku kukiwa na lori aina ya Fuso ambayo ilikuwa ikisubiri kusafirisha pikipiki hizo hadi nchini TZ. Kiongozi wa walinzi hao, alijaribu kuwatetea wafanyakazi wake bila mafaanikio kwa kuwa, imedhihirika kwamba nae huenda anahusika kwa vile, kama wanavyo sema walinzi hao walilazimishwa kufungua milango na watu 6 wenye silaha. Lakini hata hivo, haieleweki kwanini hawakufahamisha idara za uslama mapema na ilihali uwezo walikuwa nao, huku pia wakijaribu kutimka wakati walipowaona polisi wa uslama wa raia, kwa nini watimke. Uchunguzi unaendelea huku pikipiki hizo zikipelekwa kwenye idara ya polisi.

Aucun commentaire: