Waislam nchini Burundi walikuwa wamepanga kuendesha maandamano makubwa mjini Bujumbura kwa ajili ya kuwaunga mkono raia wa Palestina wanaokumbwa na matatizo wakati huu ya kuawawa kinyama huko Gaza na majeshi ya Israel. kama ilivyokuwa kawaida katika sheria na kanuni za kuendesha maandamano mea wa jiji ndie hutowa ruhusa ya kuendesha maandamano. Ombi la waislam kuendesha maandamano lilikataliwa na mea wa jij la Bujumbura Evrar GISWASWA ambae hata hivo hakutowa sababu yoyote. ilikuwa kero kubwa kwa waumini wa dini ya kiislam kukataliwa kwa maandamano hayo ambayo walikuwa wamepanga kuyanednesha katika hali baridi na tulivu. walichukuwa uamuzi wa kuendesha maandamamano hayo ndani ya majengo ya muskiti mkuu jijini Bujumbura, na baadae kugeuza uamuzi huo. haieleweki kwa nini waislam wa Burundi ndio wakataliwe kuendesha maandamano ya kupinga mashambulizi dhidi ya wayahudi dhidi ya wa Palestina, wakati ambapo ulimwengu mzima kumekuwa kukishuhudiwa maandamano ya aina hiyo ikiwemo Marekani na hata Israel kwenyewe.
dimanche 18 janvier 2009
jeudi 1 janvier 2009
WAFUNGWA WA PALIPEHUTU-FNL WATAACHIWA HURU HIVI KARIBUNI
Tarehe 31 Desemba mwaka 2008 ilikuwa imetolewa kama tarehe ya mwisho kwa pande zinazo jadiliana, yaani serikali ya Burundi na palipehutu FNL wawe wamemaliza mjadala. Uongozi wa kisiasa unaohusika na kufuatilia kwa karibu utekelezwaji wa makubaliano ya tarehe 4 Desemba baina ya serikali ya Burundi na palipehutu-FNL unaoongozwa na balozi wa afrika kusini nchini Burundi Kingsley Mamabolo umetowa tamko ambamo umesema kuendelea vema kwa majadiliano baina ya pande 2 ilikuondowa vizingiti vyote vinavyo zuia utekelzwaji kivitendo mkataba baina ya palipehutu FNL na serikali ya Burundi. Taarifa hiyo imefahamisha kwamba Kampeni ya palipehutu FNL kwa wanachama wake ili kufasiria juhudi za kubadili jina zitafanyika januari 3. juhudi za ujenzi wa kituo kingine cha kuwakusanya wapiganji wa palipehutu FNL cha Rubira zinaendelea kufanyika, na wapiganajiwa palipehutu FNL wataachiwa huru hivi karibuni. Uongozi huo wa kisiasa unaofuatilia kwa karibu utekelezwaji kivitendo mkataba wa tarehe 4 Desemba umezitaka pande mbili yaani seriklai ya Burundi na paliephutu FNL kuendelea kuonyesha utashi wa kutekeleza kivitendo mkataba huo. Kwa mujibu wa kanali Lazare Nduwayo wa tume inayo fuatilia kwa karibu utekelezwaji mkataba wa kusistisha mapigano MCVS amefahamisha kuwa hatuwa ya kuwaacha huru wafungwa wa kisisasa wa palipehutu FNL ilisainiwa jana. Sheria hiyo itapelekea kuachwa huru kwa wafungwa 246 wa palipehutu FNL
Inscription à :
Articles (Atom)