mercredi 21 juillet 2010

WAZIRI WA ULINZI NCHINI BURUNDI AOMBA KESI UFUNGULIWE DHIDI YA MWANASIASA WA MRENGO WA UPINZANI LEONARD NYANGOMA

waziri wa ulinzi nchini Burundi meja jenerali Germain Niyoyankana ameitaka mahakama nchini humo kumfungulia kesi kiongozi wa upinzani wa chama CNDD bwana léonard Nyangoma kwa kile alicho kisema kiongozi huyo amekuwa akikashifu jeshi la Burundi. Hii ni baada ya kiongozi huyo wa mrengo wa upinzani kutowa matamshi kuhusu matukio ya ndege ya kijeshi iliovurumisha ma bomu na kuwamalizia maisha watu kadhaa. waziri wa ulinzi wa Burundi amesema mwanasiasa huyo alikuwa na malengo ya kuamsha hisia mbaya za wananchi hivo wakaidi serikali pindi alipo sema kwamba serikali ya Burundi yajihusisha na mauaji dhidi ya raia. Jeshi la burundi liliendesha siku za nyuma operesheni ya kuwasaka vijana waliosadikiwa kuhusika katika vitendo tofauti vya mauaji jijini Bujumbura vikiwemo vile vya ulipuaji ma bomu. Ndege za kijeshi na manuari ya kivita ilitumiwa ili kuwazuia vijana hao ambao inasadikiwa kuwa walikuwa na dhamira ya kutimkia nchini DRC wakipitia ndani ya ziwa Tanganyika. Hadi sasa haijulikani ni watu wangapi walioyapoteza maisha katika operesheni hiyo.

1 commentaire:

FREE fonts a dit…

hello! warm greeting ^^!
your blog looks nice 0_0

by the way,
if you need to find free fonts, you can go to our website.

best regards;