
Kulingana na matokeo ya muda yaliotolewa kupitia muungano wa vyombo vya habari nchini Burundi chama tawala cha CNDD FDD cha rais waé sasa Pierre Nkurunziza kimejipatia viti 32 katika baraza la seneti huku chama UPRONA kikipata viti 2. viti hivyo 2 vyama chama UPRONA vilipatika kimoja kutoka Mkoani Bururi huku kingine kutoka jijini Bujumbura ambapo inasemekana kuwa kulikuwa na maelewano baina ya wagombea wa CNDD FDD na UPRONA. juhudu za maelewano hazikufua dafu huko Mkoani Mwaro ambapo wagombea waliochaguliwa ni kutoka chama CNDD FDD. vyama kutoka muungano wa vyama kwa ajili ya demokrasia ADC IKIBIRI havikushiriki uchaguzi tangu pale vilipo lalamikia tume huru inayo anda uchaguzi kuvuta matokeo ya uchaguzi wa viongozi wa baraza la madiwani, wajumbe ambao ndio wanaowachaguwa wanaseneti kiulingana na katiba ya Burundi. katiba ya Burundi inaamuru kuwashirika watu kutoka kabila la watwa, hivyo watwa 3 wanalazimika kuteuliwa pamoja pia na ma rais wa zamani wa Burundi.
Aucun commentaire:
Enregistrer un commentaire