BUJUMBURA LE 27.7.2010: Tume huru inayo andaa uchaguzi nchini Burundi CENI imetangaza matokeo rasmi ya uchaguzi wa wabunge uliofanyika siku ya ijumaa iliopita julay 23 mwaka 2010. Matokeo hayo yabaini kuwa chama cha CNDD FDD kimepata viti 81 bungeni huku chama UPRONA kikipata wabunge 17 na chama FRODEBU NYAKURI kikiridhika na wabunge 5. imesalia kuwateuwa wabunge 3 kutoka kabila la watwa wataotoka katika Mikoa ya Cibitoke, Karusi na Mji mkuu Bujumbura. tume hiyo inayo simamia uchaguzi CENI imesema raia walioshiriki uchaguzi wa wabunge imefikia asilimia 66. Ucahguzi wa wanasneta watazamiwa kufanyika siku ya jumanne Julay 28 ambapo kila Mkoa utwakilisha wajumbe 2 kutoka makabila ya wahutu na watutsi. tume huru CENI imetangaza kwamba vyama vya CNDD FDD na UPRONA ndivyo vitavyo wania viti vya uanaseneti. hata hivyo katika baadhi ya Mikoa chama UPRONA kimeshindwa kuorodhesha wajumbe kutoka katika kabila la wahutu. katiba ya Burundi inaagiza kwamba ma rais wa zamani wanaingia barazani moja kwa moja wakimaliza uongozi wao. Domitien Ndayizeye, Jean Baptiste, Pierre Buyoya na Ndibantunganya Syvestre ma rais wa zamani tayari ni wanaseneti.
Aucun commentaire:
Enregistrer un commentaire