mardi 27 juillet 2010

LEONARD NYANGOMA TAYARI AMEITOROKA NCHI KWA KUHOFIA USALAMA WAKE


BUJUMBURA:Mkuu wa chama cha CNDD Léonard Nyangoma akiwa pia msemaji wa muungano wa vyama kwa ajili ya demokrasia ADC IKIBIRI, vyama amvavyo vilivyo pinga matokeo ya uchaguzi wa wajumbe wa baraza la madiwani wa Mai 23, inasemeka kwamba tayari ameitoroka nchi sasa ni zaidi ya wiki. hii ni kutokana na hofu wa kutiwa nguvuni aidha kumaliziwa maisha zasema duru tofauti. Nyangoma ameitoroka nchi na kujificha kwa kuhofia maisha yake, amethibitisha hayo Alexis Sinduhije mkuu wa chama MSD kinacho jumuika katika muungano ADC IKIBIRI ambae aliliambia shirika la habari la ufaransa la AFP kwamba kiongozi huyo alionekana mara ya mwisho jijini Bujumbura Julay 20. Kiongozi huyo wa upinzani anashutumiwa na utawala baada ya kutowa tamko ambamo aliushutumu utawala kuhusika na mauaji huko Ruziba kwenye umbali wa kilometa 8 kusini mwa mji mkuu Bujumbura ambako ndege ya kijeshi na manuari vilitumiwa ilikuwasaka watu waliokuwa wamehusika katika mauaji ya wanamemba wa chama tawala CNDD FDD. waziri wa ulinzi aliomba afunguliwe mashtaka na polisi ilikuwa tayari kumtia nguvuni licha ya kinga ya muda alionayo kama mbunge.

Aucun commentaire: