jeudi 29 juillet 2010

VIONGOZI WA TARAFA WATEULIWA

Rais wa Burundi Pierre Nkurunziza amewateuwa alhamisi hii Julay 29-2010 viongozi wapya wa tarafa mbalimbali zinazo unda mikoa ua Burundi. Hata hivyo baadhi ya tarafa hazikupata viongozi wapya kwani kumekuwa na utata kuhusu uteuzi wa viongozi wa tarafa kuhusiana na tarafa ambazo madiwani kutoka muungano wa vyama kwa ajili ya demokrasia ADC-IKIBIRI walinyakua ushindi lakini baadae kukana kukaa barazani. Mathalan katika baadhi ya Mikoa ya Bujumubura vijijini jumla ya Tarafa 11, tarafa 4 pekee ndizo zimepata viongozi. Katika Manispaa ya jiji la Bujumbura tarafa 3 pekee jumla ya 13 ndizo zimewapata viongozi wapya ikiwa ni pamoja na Kamenge Buterere na Rohero. Mkoani Bururi tarafa 3 ndizo zimewapata viongozi ikiwa ni pamoja na Matana,Vyanda na Rutovu jumla ya tarafa 9. jumla ya tarafa 129, wameteuliwa viongozi 106.

Aucun commentaire: