jeudi 27 août 2009

VIONGOZI NCHINI BURUNDI WAMESHSREHEKEA MIAKA 4 KITITI WAKIWA KWENYE UTAWALA

Jana Agosti 26 viongozi walioteuliwa kwa misingi ya kidemokrasia nchini Burundi walitimiza miaka 4 kititi wakiwa kwenye utawala, baada ya uchaguzi wa mwaka 2005. Rais wa jamuhuri Pierre Nkurunziza nae pia ametimiza miaka 4 akiwa kwenye usukani wa kuiongoza Burundi. Rais Nkurunziza alizungumzia katika hutba yake jana kuhusu mustakabali mzima wa kuiongoza nchi na matatizo anayo kumbana nayo pia na mipango ijayo. Miongoni mwa yaliotekelezwa na serikali yake ni pamoja na mpango wa kudumisha amani nchini Burundi ambapo wakati huu nchini Burundi hakuna tena makundi ya uasi. Katika mipango ijayo Rais Nkurunziza amefahamsiha kuwa uchaguzi utafanyika kama ilivyo pangwa na katiba ya Burundi ameahidi kuwa uchaguzi utafanyika katika hali tulivu na ya muafaka, ameomba wale wanaopendelea kufuatilia shughuli za uchaguzi wa Burundi wangeanza mapema wakati huu. Kuhusu secta ya Afya na jamii rais Nkurunziza alitangaza mpango wa kutowa tiba kwa akinamama kuanzia mwanzo wa ujauzito hadi wanajifungua na baadae. Rais Nkurunziza ametumia fursa hiyo kukemea baadhi ya ma dactari na wauguzi ambao wamekuwa wakitowa kauli mbaya kutokana na mpango huo wa kutowa tiba pasina malipo.

Aucun commentaire: