mardi 18 août 2009

BEI YA MAFUTA YA GARI YAPANDA KWA MARA YA TENA

Serikali ya Burundi imechukuwa hatuwa ya kupandisha bei ya mafuta ya gari. Mafuta aina ya essence imepanda kutoka franka 1650 hadi 1700 lita moja huku mafuta aina ya Mazout ikipanda kutoka franka 1600 hadi 1650. hatuwa hii imechukuliwa wiki mbili baada ya kuchukuwa uamuzi kama huo, hali ambayo iliopelekea bei ya nauli za usafuri kwa abiria wanaosafiri kutoka katika tarafa mbalimbali na hata mikoani kupanda. Shirika linalo tetea haki za wanunuzi ABUCO limeihimiza serikali kufuatiliya kwa karibu bei ya mafuta ya petroli na kukomesha kuongeza bei ya mafuta hayo kwani husababisha ongezeko pia la bei ya bidha nyingine mahitajio.

Aucun commentaire: