vendredi 14 août 2009

BUNGE LA BURUNDI LAIDHINISHA MUSWADA WA SHERIA UNAOPIGA VITA MATUMIZI YA SILAHA ZA MAANGAMIZI

Bunge la Burundi limeidhinisha alhamis hii Agost 13 muswada wa sheria ya kimataifa inayo piga marufuku matumizi ya silaha za maangamizi makubwa na makombora mengine madogo madogo yanayo weza kuripuka pindi mtu anapo yasogeleya. Silaha hizo zinao uzito wa kilo 20, na zaweza pia kuripuka kabla ya kuwasili pale yalipo elekezwa. Waziri wa ulinzi wa Burundi Germain Niyoyankana alikuwa mgeni wa heshma bungeni kufafanuwa mswada huo wa sheria. Wabunge wamemuuliza umuhimu wa usainiwaji sheria hiyo kwa Bdi, waziri wa ulinzi amejibu ya kuwa sheria hiyo ni muhimu ktk lengo la kujikinga na kujihami pindi Bdi ipo kuwa imeshambuliwa. Jumla ya wabunge 98 waliohudhuria kikao hicho cha bunge, wabunge 98 wameipasisha huku mmoja akisaliya pasina kubaini msimamo wake.

Aucun commentaire: