vendredi 13 février 2009

WIZI WA KUTUMIA SILAHA WAKITIHIRI KUSINI MWA BURUNDI

Usalama mdogo unaripotiwa katika kiji cha Canda tarafani kayogoro katika mkoa wa kusini wa Makamba .Duru tawala zinasema wizi wa kutumia silaha na mitego ya kuvizia magari vimeibuka katika sehemu hiyo. Gavana wa mkoa wa makamba Pasteur BUCUMI ameiambia idhaa hii kuwa hivi majuzi polisi imefaulu kukamata guruneti , silaha moja na sare za kijeshi kwenye msako uliofanyika tarafani hapo Kayogoro. Ameongeza kuwa uchunguzi uliofanywa unaonyesha kuwa wahalifu wanatokea katika mkoa jirani wa Bujumbura vijijini.
jirani ya hapo tarafani Rumonge mkoani Bururi, Raia mmoja mfanyabiashara kwa jina Amissi Mpitabakana ameporwa kitita cha pesa zinazokadiriwa miloni 5 na laki 3 za shillingi , sarafu ya Tanzania. Kulingana na muandishi wa habari wa shirika la Burundi la habari ABP sehemu hiyo, mfanyabiashara huyo alikuwa anajiandaa kusafiri na kitita hicho hadi Tanzania kwenda kulangua bidhaa za kuuza.

1 commentaire:

Luis Portugal a dit…

Salut
Vous avez un bon blog.
Désolé de ne pas écrire plus, mais mon français écrit est mauvais.
Un câlin de mon pays, le Portugal