mercredi 18 février 2009

VIONGOZI WA KANISA WAFIA MADARAKA MBELE YA WAUMINI WAO

Hali ya kutoelewana imekuwa ikijitokeza mnamosiku zote hizi za nyuma baina ya viongozi wa kanisa la kimethodist unies katika sehemu mbalimbalia za Burundi.Tukio la karibuni ni la Hivi majuzi Mkoani Gitega viongozi wa kanisa hilo walitwangana ngumi na kuzusha vurumai na hivo kuvuruga usalama wa raia katika Mkoa huowa Gitega, pindi walifikia hali ya kuvurumishiana mawe. Kulingana na waziri wa mambo ya ndani Edouard Nduwimana amesema kuwa inaskitishwa kuona watu ambao wangelipooza nyoyo za waumini kwa kuwahutubia neno la Mungu na kuleta maendeleo, sasa ndio ambao wanavuruga usalama. Waziri huyo wa mambo ya ndani amesema kuwa walichukuwa hatuwa ya kufunga kanisa hilo baada yakutokea vurumai hizo hadi pale juhudi za upatanishi zitafikia tamati, waliopigana nao waliwekwa nguvuni na vyombo vya uslama kabla ya kufunguliwa faili na vyombo vya sheria. Waziri Edourd Nduwayo ameomba viongozi wa makanisa kuheshimu sheria zao na watakumbwa na sheria ya mwaka 1992 inamaanisha kwamba watachukuliwa hatuwa kama mashirika mengine. Amesisitizia viongozi hao wa makanisa kuheshimu sheria na kuweka mbele maendeleo na marisdhiano ya wananchi badala ya kutia mbele vyeo. Waziri huyo wa mambo ya ndani amesema kuwa kwa sasa watu wamekuwa wakishangazwa na kujiuliza vipi wahubiri sasa ndio wafia vyeo wakati cheo ni dhamana. Amesema wamo mbioni kuendesha mikutano na viongozi mbalimbali wa makanisa ili wawahamasishe kuhusu kutia mbele maridhiano badala ya kufarakiana na ilihali ni viongozi.

Aucun commentaire: