vendredi 13 février 2009

MASHIRIKA YA KICHINA YAZIDI KUJIZATITI NCHINI BURUNDI

Machimbo ya Nishati ya Nickel ya Musongati kusini mwa nchi yamekabidhiwa shirika lipya la SAMANCOR kutoka Uchina. Serikali ya Burundi ndio tu imetoa kwa shirika hilo kibali cha utafiti na shughuli za machimbo zimepangwa kuanza mnamo kipindi cha miaka miwili ijayo.
Hayo yamefahamishwa na waziri wa BDI wa nishati na madini Samuel Ndayiragije. Waziri huyo amesema uwanja huo wa machimbo ya madini ya Nickel ulikuwa wazi baada ya serikali ya Burundi kuvunja kandarasi ya shirika la Andover tangu mwaka 2007.

Aucun commentaire: