vendredi 13 février 2009

WAALIMU WA BUTERERE WAANZISHA MGOMO

Waalimu wa shule za msingi na upili tarafani Buterere kaskazini mwa jiji la Bujumbura wameanzisha mgomo wa kususia kutoa visomo wakidai wapewe kwanza viwanja vya ujenzi walivyoahidiwa na serikali. Waalimu hao wanaojumuika kwenye mashirika ya waalimu ya STEB na CONAPES wanaonyeshea hasa kidole Baraza la madiwani tarafa hapo ,kugawa viwanja hivyo kwa watu binafsi badala ya kuwapatishia waalimu. Mwenzangu Karim Nkeshimana amezungumza na Jean Bosco Ndarusanze , mwalimu wa shule la upili wa Buterere. Pamoja na mgomo huo , kazi ya dharura imekuwa inafanywa ikiwa ni pamoja na kutoa visomo kwa wanafunzi wa madarasa ya sita na ya kumi yanayotahiniwa kitaifa. Tumejaaribu kuwasiliana na wakuu wa tarafa ya Buterere kutoa muanga zaidi kuhusiana na hali hiyo pasina mafaanikio.

Aucun commentaire: