mercredi 9 septembre 2009

POLISI YA USALAMA WA RAIA HAIJA FAULU KUWAKAMATA MAJAMBAZI WALIOJARIBU KUMMALIZIA MAISHA MSANII JOHN CHRIS


Hadi sasa polisi haijafaulu kuwakamata watu waliojaribu kummalizia maisha msanii John Chris wakati wa likizo yake mjini Bujumbura. John Chris alinusurika katika tukio lililo endeshwa na watu ambao hawajajulikana katika usiku wa kuamkia jumanne Septemba Mosi mwaka huu. Kama alivyo eleza mwenyewe kwenye Vyombo vya habari Msani huyo mwenye asili ya Burundi ambae sasa anaishi Mjini Bruxels Ubelgiji alikuwa pamoja na familia katika sherehe za kuagana kwa kuwa alikuwa amehitimisha likizo yake mjini Bujumbura, wakati alipo toka akiwa na walinzi wake 2, alijieleza sehemu kujisaidia, alipo rudi ndipo akakuwa watu 2 waliokuwa na bastola tayari kuziweka kichwani kwa walinzi aho ambao walikuwa ni askari polisi waliovalia nguo za kiraia. Alipo fika nae akawekwa bastola kichwani na kuambiwa aondowe kila kilicho mfukoni mwake, hakusita kufanya hivo kama alivyo eleza. Lakini mmoja kati ya walinzi wake alijaribu kujiokowa kwa kuridi nyuma ili apate jinsi ya kutowa bastola ambayo aliokuwa nayo ili awashambulie majambazi hao, huku mwengine akimsukuma msanii huyo kama kumponyesha. Mmoja kati ya majambazi hao alirusha rusase zikampata mmoja kati ya walinzi kwenye mbavu. Majamabazi hao walitimka baada ya kuona kwamba mambo yamekuwa magumu. Askari polisi huyo afya yake sio mbaya anaendelea kupata matibabu kwenye Hospitali mojawapo jijini Bujumbura.

1 commentaire:

www.Gatto999.it a dit…

Ciao form Italy
=^.^=