samedi 12 septembre 2009

WANASIASA NCHINI BURUNDI WATOFAUTIANA KUHUSU SHERIA YA UCHAGUZI

BUJUMBURA: Kumekuwa na hisia tofauti baina ya wanasiasa nchini Burundi kuhusiana na sheria ya uchaguzi iliopasishwa bungeni usiku wa alhamis kuamkia ijumaa septemba 11, 2009. Chama Sahwanya FRODEBU kimesema kufurahishwa na hatuwa hiyo ya kupasisha sheria ya uchaguzi bungeni, lakini hata hivo mwenyekiti wa chama SAHWANYA FRODEBU Leonce Ngendakumana amesema kuwa na wasiwasi hasa kwamba kadi moja ya uchaguzi iliokuwa ikitetewa na chama hicho haikupasishwa kaika muswada huo. upande wake msemaji wa chama FNL Bosco HAVYARIMANA amesema kuwa wabunge wamekwenda kinyume kabisa na maafikiano waliokuwa wamekubaliana siku za nyuma. kiongozi huyo amesema kuwa kiwango cha dhamana kinacho takiwa kwa wagombe viti mbalimbali vya uchaguzi hakina sababu za kuwepo. upande wake mwenyekiti wa chama CNDDLéonard Nyangoma amesema ni aibukubwa sana kwa taifa la Burundi. upane wake amesema sheria hiyo ya uchaguzi inakuja kurejesha nyuma hatuwa za demokrasia nchini Burundi ukilinganisha na sheria.

Aucun commentaire: