PALIPEHUTU/FNL WAPEWA CHAKULA KWA MARA NYINGINE TENA.
Bujumbura le 14/7/2008. Shughuli za kuwapa chakula wapiganaji wa palipehutu/FNL zimeanzishwa tena jumatatu hii. Hayo yamefahamishwa na msemaji wa kundi hilo Pasteur HABIMANA. Akizungumza katika mahojiano kupitia njia ya simu kwenye redio Burundi, Pasteur HABIMANA alisema kuwa muakilishi wa msuluhishi nchini Burundi Kingslay Mamaboulo alishindwa kuzibiti hali ya mambo wakati alipo safiri muakilishi maalum wa umoja wa Afrika nchini Burundi Mamadou Ba na kutofahamisha mapema kwamba chakula kiliopo kimekwisha. Kusitishwa kwa shughuli hizo kulipelekea wapiganaji wa palipehutu/FNL kuingia ndani ya majumba ya raia na kupora chakula. Msemaji wa palipehutu/FNL ameitolea mwito jamii ya kimataifa kuongeza idadi ya chakula wanacho pewa wapiganaji wa kundi hilo wakati huu. Kama alivyo fahamisha, kila mpiganaji hupewa chakula mara moja kwa siku, sawa na kilo 4 kwa wiki.
WATUHUMIWA 6 WA MAUAJI YA DACTARI KASSY MANLAN WAACHIWA HURU.
Bujumbura le 14/7/2008 Watuhumiwa 6 wa mauaji ya aliekuwa muakilishi mkaazi wa shirika la afya ulimwenguni nchini Burundi, Dactari Kassy Manlan, wameachiwa huru. Korti kuu ya sheria iliamuru watuhumiwa hao wafunguliwe tangu juni 12, baada ya kufungwa kwenye jela kuu la Mpimba tangu Novemba 2003. watuhumiwa hao 6 ambao ni pamoja na Gerard ntunzwenayo, Emile Manisha, Aloys Bizimana, Japhet Ndayegamiye, Expert Bihumugani na Athanase Bizindavyi, wamebaini kuridhishwa na kufunguliwa kwao. hata hivo Pierre Claver Mponimba kiongozi wa shirika linalo tetea haki za wafungwa amesema kwamba kufunguliwa kwa watuhumiwa hao ni pigo kubwa kwa vyombo vya sheria nchini Burundi, kiongozi huyo amebaini kuwa kesi hiyo lazima ifikie kileleni na wahusika lazima watambulike. Jamii ya warundi wanajiuliza wakati huu kuhusu hatma ya kesi hiyo baada ya watuhumiwa hao kukutwa bila hatia. Upande wake Wakili Marc BIRIHANYUMA amesema kusikitishwa kuona vyombo vya dola na vile vya sheria vimeshindwa kuendesha uchunguzi kama ipasavyo kuhusu kifo cha hayati Kassy Manlan ili warundi na jamii ya kimataifa watambuwe ukweli zaidi kuhusu kifo hicho ambacho kina tatanisha. Inavyo dhihirika wakati huu, utafkiri kwamba hayati Manlan alijiua mwenyewe na baadae kenda kujitupa katika ziwa tanganyika, amesema hayo mwanasheria huyo.
Bujumbura le 14/7/2008. Shughuli za kuwapa chakula wapiganaji wa palipehutu/FNL zimeanzishwa tena jumatatu hii. Hayo yamefahamishwa na msemaji wa kundi hilo Pasteur HABIMANA. Akizungumza katika mahojiano kupitia njia ya simu kwenye redio Burundi, Pasteur HABIMANA alisema kuwa muakilishi wa msuluhishi nchini Burundi Kingslay Mamaboulo alishindwa kuzibiti hali ya mambo wakati alipo safiri muakilishi maalum wa umoja wa Afrika nchini Burundi Mamadou Ba na kutofahamisha mapema kwamba chakula kiliopo kimekwisha. Kusitishwa kwa shughuli hizo kulipelekea wapiganaji wa palipehutu/FNL kuingia ndani ya majumba ya raia na kupora chakula. Msemaji wa palipehutu/FNL ameitolea mwito jamii ya kimataifa kuongeza idadi ya chakula wanacho pewa wapiganaji wa kundi hilo wakati huu. Kama alivyo fahamisha, kila mpiganaji hupewa chakula mara moja kwa siku, sawa na kilo 4 kwa wiki.
WATUHUMIWA 6 WA MAUAJI YA DACTARI KASSY MANLAN WAACHIWA HURU.
Bujumbura le 14/7/2008 Watuhumiwa 6 wa mauaji ya aliekuwa muakilishi mkaazi wa shirika la afya ulimwenguni nchini Burundi, Dactari Kassy Manlan, wameachiwa huru. Korti kuu ya sheria iliamuru watuhumiwa hao wafunguliwe tangu juni 12, baada ya kufungwa kwenye jela kuu la Mpimba tangu Novemba 2003. watuhumiwa hao 6 ambao ni pamoja na Gerard ntunzwenayo, Emile Manisha, Aloys Bizimana, Japhet Ndayegamiye, Expert Bihumugani na Athanase Bizindavyi, wamebaini kuridhishwa na kufunguliwa kwao. hata hivo Pierre Claver Mponimba kiongozi wa shirika linalo tetea haki za wafungwa amesema kwamba kufunguliwa kwa watuhumiwa hao ni pigo kubwa kwa vyombo vya sheria nchini Burundi, kiongozi huyo amebaini kuwa kesi hiyo lazima ifikie kileleni na wahusika lazima watambulike. Jamii ya warundi wanajiuliza wakati huu kuhusu hatma ya kesi hiyo baada ya watuhumiwa hao kukutwa bila hatia. Upande wake Wakili Marc BIRIHANYUMA amesema kusikitishwa kuona vyombo vya dola na vile vya sheria vimeshindwa kuendesha uchunguzi kama ipasavyo kuhusu kifo cha hayati Kassy Manlan ili warundi na jamii ya kimataifa watambuwe ukweli zaidi kuhusu kifo hicho ambacho kina tatanisha. Inavyo dhihirika wakati huu, utafkiri kwamba hayati Manlan alijiua mwenyewe na baadae kenda kujitupa katika ziwa tanganyika, amesema hayo mwanasheria huyo.
1 commentaire:
Who knows where to download XRumer 5.0 Palladium?
Help, please. All recommend this program to effectively advertise on the Internet, this is the best program!
Enregistrer un commentaire