Watu 3 wameuawa Mkoani Kirundo katika kijiji cha Renga zone ya Mukerwa tarafa ya Busoni katika usiku wa kuamkia alhamisi hii saa tatu na robo pindi majambazi waliokuwa na silaha walipo vamia familia moja. Miongoni mwa hayati hao ni baba na mkewe pamoja na mama yake. Katika tukio hilo dada wa hayati huyo alijeruhiwa.
Usalama mdogo umeripotiwa pia katika kijiji cha Migera Mkoani Nyabihanga. Watu wzenye silaha waliivamia nyumba ya mfanyabiashara mmoja ajulikanae kwa jina la Ntabahungu Gaspard. Baada ya kuwajeruhi watu 2 na risase wahalifu hao ndipo walianza kuwapora watu simu za mkononi, redio na pesa ambazo haijulikani idadi yake. Katika usiku huohuo mwananchi Nkurunziza Evariste wa kijiji cha Bugera tarafani Ndava alipigwa risase na wahalifu magotini na baadae wakatimka.
Usalama mdogo umeripotiwa pia katika kijiji cha Migera Mkoani Nyabihanga. Watu wzenye silaha waliivamia nyumba ya mfanyabiashara mmoja ajulikanae kwa jina la Ntabahungu Gaspard. Baada ya kuwajeruhi watu 2 na risase wahalifu hao ndipo walianza kuwapora watu simu za mkononi, redio na pesa ambazo haijulikani idadi yake. Katika usiku huohuo mwananchi Nkurunziza Evariste wa kijiji cha Bugera tarafani Ndava alipigwa risase na wahalifu magotini na baadae wakatimka.
Aucun commentaire:
Enregistrer un commentaire