kumetokea hali ya mvutano kati ya Polisi wa uslama wa raia nchini Burundi na wakimbizi wa congo wa kabila la Banyamulenge. Tukio hilo limetokeya ktk kambi ya Gihinga iliyo mkoani Mwaro kati kati mwa Bdi umbali wa kilometa 70 hivi na mji mkuu Bujumbura, ambako askari polisi wamewafiatuliya risase wakimbizi banyamulenge na wawili miongoni mwao kujeruhiwa, huku wengine watatu wakizirayi kutokana na miliyo ya risase kambini hapo Gihinga. Kambi hiyo ya Gihinga ilikuwa imewapa hifadhi wakimbizi Banyamulenge 2317 kutoka nchi jirani ya RDC. Septemba 21 ndipo Shirika la UM linalo wahudumiya wakimbizi UNHCR liliamuru kusitisha huduma zake zote kwa wakimbizi hao, baada ya wakimbizi hao kupinga kuhamishiwa ktk kambi ya bwagiriza iliyo ktk mkoa wa Ruyigi mashariki mwa Bdi kwenye mpaka na Tanzania. Septemba 30 shirika la UNHCR lilitangaza kuwa kambi ya Gihinga imefungwa licha ya wakimbizi hao kusaliya kambini huku miongoni mwao 264 wakikubali kuhamishiwa bwagiriza mkoani Ruyigi. Hatua hiyo ilipelekeya wakimbizi hao kuchukuwa uwamuzi wa kurudi kwa mguu nchini kwao RDC, hatua ambayo imeanza kutekelezwa jumanne hii.
Aucun commentaire:
Enregistrer un commentaire