mercredi 3 septembre 2008

POLISI YA USALAMA WA RAIA YAMMALIZIA MAISHA JAMBAZI BAADA YA KUWAPORA HABIRIA KWENYE BARABARA ITOKAYO BUJUMBURA KUELEKEA GATUMBA
Majambazi wenye silaha waliendesha mtego siku ya jumamosi tarehe 30/8/2008, kwenye barabara itokayo mjini Bujumbura kuelekea tarafani Gatumba. basi moja la habaria lilianguka kwenye mtego huo. habiria waliokuwemo ndani ya basi hilo waliporwa pesa, simu za mkononi na vitu mbalimbali vya thamani waliokuwa navyo. baada ya shambulio hilo, jeshi la taifa eneo hilo liliingia kati na kumuua jambazi mmoja ambae alikuwa amevalia sare za jeshi la Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo. Hata hivo raia wa Gatumba waliokuja kushuhudia tukio hilo walithibitisha kwamba jambazi huyo alieuliwa ni mkaazi wa kata ya Gatumba. mnamo siku zote hizi za nyuma kumekuwa na hujuma mbalimbali ambazi zimekuwa zikiendeshwa na majambazi wenye silaha katika barabara tofauti zinazo toka mjini Bujumbura kuelekea mikoani.

2 commentaires:

MULTISERVICE a dit…

mbona mmekuwa hamtupi habari kwa wakati kumetokea nini? tulikuwa tukipendezwa sana na namna jinsi mnavyotupa habari

Anastácio Soberbo a dit…

Hello, I like this blog.
Sorry not write more, but my English is not good.
A hug from Portugal

Olá, goût très du Blogue.
Excuse ne pas écrire plus, mais mon français n'est pas bon.
Une accolade depuis le Portugal