jeudi 25 septembre 2008

Shughuli za ujenzi wa soko la Buyenzi zimekamilika. kinacho salia ni shirika la mamlaka ya maji na umeme REGIDESO paomja na manispaa ya jiji la Bujumbura kushughulikia maswala ya umeme na maji katika soko hilo muhimu kwa uchumi wa nchi. hayo yamethibitishwa na Anatole MPERAMIHIGO ambae alikuwa akisimamia shughuli za ujenzi wa soko hilo. Lakini hata hivo kumekuwa na uvumi kwamba shughuli za ujenzi wa soko hilo la Ruvumera zilikamilika tangu kitambo, uzinduzi rasmi unacheleweshwa kutokana na hali ya viongozi wa kuu serikali kujipa viwanja zaidi ya vitano kila mmoja ambapo waliokutwa katika soko hilo kabla hata halijakarabatiwa huenda wakakosa viwanja.

Aucun commentaire: