Waislam nchini Burundi walikuwa wamepanga kuendesha maandamano makubwa mjini Bujumbura kwa ajili ya kuwaunga mkono raia wa Palestina wanaokumbwa na matatizo wakati huu ya kuawawa kinyama huko Gaza na majeshi ya Israel. kama ilivyokuwa kawaida katika sheria na kanuni za kuendesha maandamano mea wa jiji ndie hutowa ruhusa ya kuendesha maandamano. Ombi la waislam kuendesha maandamano lilikataliwa na mea wa jij la Bujumbura Evrar GISWASWA ambae hata hivo hakutowa sababu yoyote. ilikuwa kero kubwa kwa waumini wa dini ya kiislam kukataliwa kwa maandamano hayo ambayo walikuwa wamepanga kuyanednesha katika hali baridi na tulivu. walichukuwa uamuzi wa kuendesha maandamamano hayo ndani ya majengo ya muskiti mkuu jijini Bujumbura, na baadae kugeuza uamuzi huo. haieleweki kwa nini waislam wa Burundi ndio wakataliwe kuendesha maandamano ya kupinga mashambulizi dhidi ya wayahudi dhidi ya wa Palestina, wakati ambapo ulimwengu mzima kumekuwa kukishuhudiwa maandamano ya aina hiyo ikiwemo Marekani na hata Israel kwenyewe.
Aucun commentaire:
Enregistrer un commentaire